Wachezaji wa Yanga wakishangilia Ushindi - Uwanja wa Kirumba Mwanza
Yanga ilishinda katika Mchezo huo kwa Magoli 3 - 1
Magoli
mawili ya Kipindi Cha kwanza ya Yanga Dakika ya Pili la Didier Kavumbagu na
Mbyu Twite lilopatikana Dakika ya 21 yalifanya Timu ya Jangwani iende Mapumziko
ikiwa Kifua Mbele kwa magoli Mawili. Kipindi Cha pili kilipoanza kilishuhudia
Mchezaji Jerry Tegete akifumania nyavu za Toto Afican katika Dakika ya 69 na
kuhitimisha Mvua ya Magoli kutoka kwa vijana hawa Jangwani. Goli la Said
Mussa wa Toto Africa ndilo lilipeleka kifuta Machozi kwa Vijana hawa wa Mwanza
ambao walivunja rekodi ya kuifunga timu hii ya Jangani katika Msimu uliopita
Matokeo
haya ni Faraja kwa timu hii lakini hasa
kwa Kocha Muholanzi Johannes Brandts aliyetokea APR Rwanda kuja
kuvaa viatu vyaTom
Saintfiet ambaya mkataba wake ulikatishwa kutokana na matokeo yasiyoridhisha.
Matokeo haya yanaifanya Yanga
kujiongezea pointi Tatu na kuwa na Pointi 11 kwenye Msimamo wa Ligi
Furaha kwa Wachezaji wa Yanga Baada ya Kuifunga Toto Africa
Yanga ilishinda katika Mchezo huo kwa Magoli 3 - 1
No comments:
Post a Comment