WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Thursday, May 3, 2012

Ni Manchester City….

Baada ya Shauku, hamasa na kukamiana, hatimaye Goli la Vincent Kompany liliamua Mshindi wa Manchester Derby. Ushindi huu umewapaisha Manchester City kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kutwaa kwa mara nyingine usukunani wa ligi. Goli hili lililofungwa mwishoni mwa kipindi cha pili kwa kuunganisha mpira wa kona lilidumu mpaka mwisho wa mchezo.
Kompany akiunganisha mkwaju wa Kona kimiani
Kompany akifurahia goli lake la  kwa shangwe


Hebu tujikumbushe Goli hilo lilivyofungwa….



Matokeo haya yanazidi kufanya kinyang’anyiro cha ubingwa wa kombe la ligi ya Uingereza kuwa gumu sana huku ukiipa nafasi kubwa Manchester City endapo timu zote mbili (Manchester city na Manchester United) zitashinda katika mechi zilizobaki.

Matokeo haya yanazifanya timu hizi mbili kufungana kwa pointi na kutofautiana kwa idadi kubwa ya Magoli ambayo yanaiweka Manchester City katika Nafasi nzuri zaidi.

Manchester City inataka kutwaa ubingwa wa mashindano haya kwa mara ya kwanza tangu ilipofanya hivyo mwaka 1968 huku wakiwa na mechi ngumu mbele yao dhidi ya New Castle United.

No comments:

Post a Comment