Leo
tarehe 3 Mei ni siku ya uhuru wa
vyombo vya habari duniani ambayo huadhimishwa ulimwenguni kote. Siku hii ili
ilitangazwa rasmi na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuamsha Ufahamu wa Umuhimu
wa Uhuru wa Habari na kuzikumbusha Serikali Wajibu wao katika Kuheshimu na Kusimamia
Uhuru wa Kujieleza. Msingi wa Wajibu huu unapatikana katika katika Kifungu cha
19 cha Tamko la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lililotolewa Ufaransa mwaka
1948 baada ya Matukio ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Pamoja
na Siku hii kuwa na msingi wa kimataifa, Waandishi wa Magazeti wa Afrika waliokutana Windhoek, Namibia katika
semina iliyoandaliwa na UNESCO walitoa Tamko la Windhoek la Misingi ya Uhuru wa
Habari mwaka 1991.
Hivyo
siku hii ya Uhuru wa Vyombo vya habari inatokana na misingi mbalimbali
madhubuti inayolenga kuhakikisha Heshima, Umuhimu na ulinzi wa misingi ya Uhuru
wa habari.
Ofisi za UNESCO Makao Makuu
UNESCO
huwa inaadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari kwa kutoa Tunzo ya
Guillermo Cano kwa mtu binafsi, kampuni au taasisi iliyotoa mchango mkubwa
kulinda na kutetea uhuru wa habari popote duniani hasa pale utetezi huu
unapotokea kwenye mazingira hatarishi. Tunzo hii ilianza kutolewa mwaka 1997
ambapo kamati ya nguli 14 weledi katika tasnia ya Habari wanoachaguliwa na Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO na kutumikia
kipindi cha miaka mitatu, hupendekeza
jina la atakayepokea Tunzo katika mwaka husika. Jina hilo hutokana na mapendekezo
kutoka Taasisi zisizokuwa za kiserikali za kikanda na kimataifa
zinazojishughulisha na Uhuru wa Habari na nchi wanachama wa UNESCO.
Kamati iliyohusika katika uteuzi wa jina la mpokea Tunzo wa Mwaka huu inaongozwa na Diane Senghor kutoka Senegal ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa wa Taasisi ya Kuendeleza Utamaduni wa Kidemokrasia na Majadiliano. Wengine katika kamati hiyo ni Alexandra Föderl-Schmid (Austria), Bulbul Monjurul Ahsan (Bangladesh), Miklos Haraszti(Hungary), Ognian Zlatev (Bulgaria), Daniel Santoro (Argentina), Steven Gan (Malaysia), Fatuma Noor (Kenya), Rossana Fuentes-Berain (Mexico), Rana Sabbagh, (Jordan), Gamal Eid (Misri), Florence Aubenas (Ufaransa).
Tunzo hiyo imepewa jina la Guillemo Cano Isaza ambaye alikuwa Mwandishi wa habari aliyeuwawa mbele ya ofisi za gazeti analoliandikia la El Espectador mwaka 1986 baada ya kuanzisha kampeni ya ushawishi wa wauza madawa ya kulevya katika siasa nchini Colombia.
Mwaka
huu, 2012, Siku hii ya Uhuru wa Vyombo vya Habari inaadhimishwa Tunisia ambapo
Mkurugenzi wa UNESCO, Irine Bokova amemtangaza, Mwanaharakati na Mwandishi wa Habari
wa Azberjani, bwana Eynulla Fatullayev (35)
kuwa mshindi wa Tunzo ya Guillemo Cani.
Eynulla Fatullayev (35) Mshindi wa Tunzo ya Guillemo Cani mwaka 2012
Eynulla
Fatullayev alikuwa Mhariri Mkuu na Muasisi wa Gazeti la wiki la “Realny
Azerbaijan” lililokuwa likiandikwa katika lugha ya Kirusi na gazeti la kila
siku la “Gundalik Azarbaycan” lililokuwa likiandikwa katika lugha ya
Kiazabejaini.
Azerbejaini
ni nchi inayopatikana katika ya Bara la Asia na Ulaya ikipakana na bahari ya
Caspian, Urusi, Georgia, Armenia na Urusi. Mara nyingi nchi hii imekuwa
ikihesabiwa kama nchi ya Ulaya kutokana na kuwa Mwanachama wa Baraza la Ulaya Tangu mwaka 2001 ingawaje
kijografia huwa inahesabiwa kama sehemu ya Asia Magharibi.
Katika
taaluma yake Eynulla Fatullayev amekuwa akipigania, kutetea na kusimamia Uhuru wa
Habari na Uhuru wa Kujieleza. Harakati hizi zilisababishwa kutiwa hatiani na
kufungwa mwaka 2007 mpaka alipoachiwa kwa msamaha wa Raisi siku ya kuadhimisha
sikukuu ya Jamhuri ya Azerbajaini tarehe
26 Mei mwaka 2011. Mara tu baada ya kuachiwa huru alianzisha taasisi isiyokuwa
ya serikali “Public Union for Human Rights”. Tunzo hii inakwenda kwake kwa
kutambua mchango wake kwa kuzingatia misingi na vigezo vilivyowekwa katika
kumpata mshindi.
Mpaka
sasa tunzo hii imeshakwenda kwa wanahabari 16 wakiwemo wawili kutoka katika
bara la Afrika. Waandishi na wanaharakati wengine waliowahi kupata tunzo hii tangu
ilipoanzishwa ni pamoja na:
1.
Gao
Yu (China, 1997)
2.
Christina
Anyanwu (Nigeria, 1998)
3.
Jesus Blancornelas (Mexico, 1999)
4.
Nizar
Nayyouf (Syria, 2000)
5.
U
Win Tin (Myanmar, 2001)
6.
Geoffrey Nyarota (Zimbabwe, 2002)
7.
Amira Hass (Israel, 2003)
8.
Raúl Rivero (Cuba, 2004)
9.
Cheng
Yizhong, (China, 2005)
10. May Chidiac (Lebanon,
2006)
11. Anna Politkovskaya
(Russian Federation, 2007)
12. Lydia Cacho (Mexico, 2008)
13. Lasantha Wickrematunge
(Sri Lanka, 2009)
14. Mónica González Mujica
(Chile, 2010)
15. Ahmad Zeidabadi (Iran,
2011)
Huku
ndiko ilikotoka tunzo ya Guillemo Cano ambayo hutolewa kila mwaka katika
maadhimisho ya Siku ya Vyombo vya habari duniani.
Hongera wanahabari wote Duniani...
Hongera wanahabari wote Tanzania...
(Habari kwa hisani ya UNESCO na Wikipedia)
No comments:
Post a Comment