WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Friday, May 4, 2012

HATIMAYE BARAZA LA MAWAZIRI LATANGAZWA RASMI


Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akitangaza Baraza la Mawaziri Leo Mei 4, 2012

Baada ya Siku kadhaa za mjadala kuhusu Baraza la Mawaziri kufuatia mjadala ulioanzishawa Bungeni kufuatia ripoti ya Mkaguzi mkuu wa Serikali, hatimaye leo yametimia.

Baraza jipya limeshuhudia Baadhi ya Mawaziri waliokuwa wakitajwa kwenye ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na zile za Kamati za kudumu za Bunge kuwa Wzara zao zilibainika kuwa na vitendo vya ubadhirifu wa mali ya umma wakiondolewa katika nafasi zao.

Pamoja na hao pia Baraza hili tofauti na lililokuwepo linakosa sura maarufu za Mawaziri wafuatao:

1.      Mustafa Mkulo aliyekuwa Waziri wa Fedha

2.      William Ngeleja aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini

3.      Cyril Chami aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

4.      Omari Nundu aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi

5.      Dkt. Hadji Hussein Mponda Aliyekuwa Waziri wa Afya

6.      Ezekiel Maige aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii,

7.       Dr. Athuman Mfutakamba aliyekuwa Naibu Waziri Wa Uchukuzi
Mustafa Mkulo


William Ngeleja

Cyril Chami

Omari Nundu



Dokta Hadji Mponda

Ezekiel Maige


Dr. Athumani Mfutakamba
Aidha Baraza hilo limeshuhudia Mbunge machachari wa jimbo la Bumbuli January Makamba akiteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

Januari Makamba
Aidha uteuzi huu na mabadiliko haya yameshuhudia baadhi ya Manaibu Waziri wakipanda na kuwa Mawaziri kamili kama vile:

1.      Dr. Harrison Mwakyembe, aliyekuwa Naibu Waziri, Wizara ya Ujenzi anakuwa Waziri wa Uchukuzi

2.    Dr. Fenella E. Mukangara aliyekuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo sasa anakuwa Waziri kamili katika Wizara hiyohiyo na

3.   Khamis Kagasheki aliyekuwa Naibu Waziri Mambo ya Ndani anakuwa Waziri wa Maliasili na utalii


Dr. Harrison Mwakyembe


Dr. Fenella E. Mukangara


Balozi Khamis Kagasheki

Orodha kamili ya Baraza la Mawaziri iliyotangazwa na Mheshimiwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu leo tarehe 4 Mei 2012 ni:

1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,

2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

3. OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

4. WIZARA
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,

Waziri wa Ujenzi
Dr. John P. Magufuli, Mb.,

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,

Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,

 Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,

Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,

Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,

Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,

 Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,

Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,

Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,

Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,

5. NAIBU MAWAZIRI

OFISI YA RAIS
Hakuna Manaibu Wazari

6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

7. OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

 8. WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,

 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,

Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,

Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,

Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,

Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,

Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Mawaziri hawa wateule wataapishwa siku ya Jumatatu Tarehe 7 Mei 2012

Na sisi tulikuwepo pale ikulu....



No comments:

Post a Comment