Mwisho wa Msimu wa ligi huja na msisimko katika Nyanja
mbalimbali ikiwemo ajira, usajilii, mipango na mikakati kwa ajili ya msimu ujao
n.k Haya yote hutokana na uzoefu uliopatikana katika msimu uliokwisha. Msisimko
huu umemkuta pia Meneja wa Liverpool bwana Kenny Daglish!
Kenny Daglish
(Picha kwa Hisani ya Gatee Images)
Baada ya miezi 18 akiwa meneja wa kikosi cha Liverpool, Bwana
Kenny Daglish, amefungashiwa virago na wenye mali John Henry na Tom Werner mjini
Boston ili akatafute Riziki sehemu nyingine, kwani Riziki popote… Wenye
mali hawakuridhishwa na matokeo ya Msimu huu ambapo zaidi ya Liverpool kufika
fainali ya FA na kuchukua Kombe la Carling, timu hiyo imemaliza ligi kuu ya
England ikiwa nafasi ya nane huku ikipoteza michezo mingi na kutokubaliana na
sababu zilizokuwa zikitolewa hasa pale iliposhindwa kuqualify kuingia katika
Nne Bora ili kujihakikishia ushiriki katika kombe la Mabingwa.
Kufa kufaana kwa ni Majina kama Roberto Martinez Kocha Mkuu wa
Wigan na Rafael Benitez Kocha wa zamani wa Liverpool yameanza kutajwa
kuziba nafasi inayoachwa wazi na Kenny Daglish......
Roberto Martinez
Rafael Benitez
Haya ndiyo ni kati ya mengi yatokanayo na Msimu wa ligi
2011/12....
go to hell KD
ReplyDeleteMategemeo yalikuwa makubwa sana baada ya KD kuingia Liverpool lakini Matumizi katika usajili na performance ya timu; vilionyesha wazi kuwa kama Livepool inataka kutunza heshima yake basi mabadiliko ilikuwa ni lazima....
Delete