WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Wednesday, May 16, 2012

Patrick Mafisango Afariki kwa ajali ya Gari

Patrick Mafisango
Tumepokea habari  kutoka Radio One kuwa kiungo wa Simba, Patrick Mafisango (25) amefariki kwa ajali ya Gari, Tazara Dar es Salaam Leo asubuhi. Mafisango alikuwa akirejea nyumbani akitokea kwenye burudani ya Muziki.

Patrick Mutesa Mafisango ambaye ni Raia wa Rwanda,alikuwa akichezea timu ya Azm kabla hajajiunga na timu ya wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club. Patrick mafisango aliwahi kuzichezea timu kama Atraco na APR za Rwanda Huku akiwa kiungo katika timu ya Taifa ya Rwanda, Amavubi.
 Patrick Mafisango akiwa Azam FC ya Dar es Salaam
Akiwa Azam FC
Mafisango wakati akiwa na imu ya Jeshi APR ya Rwanda
Kapteni wa Timu ya APR Patrick Mafisango akiwa ameshikilia kombe la Cecafa Kagame Cup 2010 baada ya kuifunga St. George 
Umaarufu wa Mchezaji huyo Kiungo ulizidi kuongezeka akiwa na Timu ya Simba hasa katika msimu huu ambapo upachikaji wake wa magoli na Pasi zilizozaa magoli.



Mwenyezi Mungu aliaze Roho ya Marehemu Patrick Mafisango Peponi

No comments:

Post a Comment