WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Saturday, May 19, 2012

Leo ni Fainali Kombe la Mabingwa..



Ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kuikutanisha miamba miwili ya soka Bayern Munich na Chelsea imewadia. Timu hizi zilizofanikiwa kuingia katika fainali zitakutana usiku huu pale Fußball Arena München (Allianz Arena) -Nyasi zitawaka moto!

Timu hizi zimefikia hatua hii baada ya kushinda katika michezo yao ya fainali ambapo Chelsea ambayo inakaribishwa Mjini Munich ilikiondoa kigogo cha Soka na klabu bingwa ya dunia, Barcelona ya Hispania huku Bayern Munich ikiiondoa timu nyingine ngumu ya Hispania Real Madrid.

Jiji la Munich limetawaliwa na homa ya mchezo huu wa fainali huku mashabiki wa timu zote mbili wakiwa wameifunika mitaa ya Munich wakiwa wamevalia jezi za timu zao huku wakipeperusha bendera kuzitakiwa ushindi timu zao.
Homa hii haipo tu kwa mashabiki na wachezaji bali ipo kwa kiasi kikubwa kwa makocha wa timu hizi; Jupp Heynckes wa Bayern Munich na  Roberto Di Matteo wa Chelsea FC



Bayern Munich wanaingia uwanjani leo wakiwa na historia katika mashindano haya ambapo wamewahi kushiriki fainali kama hizi na kuchukua ubingwa. Bayern Munich wameshachukua ubingwa wa kombe hili mara nne (4) na kuwa washindi wa Pili mara nne. Hii ni mara ya tano Bayern Munich wanakutana na timu ya Chelsea katika ligi ya Mabingwa.

Chelsea walikaribia kunyakuwa ushindi wa kombe hili pale ilipokutana na timu ya Manchester United na ikakosa ubingwa huo pale John Terry alipokosa Penati. Chelsea imeshawahi kufikia Nusu fainali na robo fainali bila kuchukua ubingwa mara nyingi katika ligi ya mabingwa.

Chelsea leo watamkosa John Terry kutokana na kadi nyekundu aliyoipata walipokutana na Barcelona katika Mchezo wa Nusu fainali. Chelsea bado inajivunia wachezaji wake kama Jose Bosingwa , Raul Mirlaes , Ashley Cole , Mata , Fernendo Torres na Frank Lamaparad t huku wachwzaji kama Dider Drogba , Salmon Kalou na Studdrige watachangia kuimarisha makali ya timu hiyo .

Drogba amesema kuwa Chelsea imesubiri kwa miaka mine kufikia hapa na kuchukua ubingwa, kitu muhimu kwake kwa sasa ni ushindi wa timu yake.
Bayern Munich wana kikosi kizuri leo wakijivunia hazina ya wachezaji kama  Frank Riberey , Arjen Robben , Mario Gomez , Tomas Mullar , na Bastin Schewnstiger.  

Wachezaji wote hawa wataleta burudani kubwa pale
Fußball Arena München (Allianz Arena) na chochote kinaweza kutokea

Tunategemea burudani kuu

Tunamsubiri mshindi

Tunawatakia heri  - Tupeni raha

No comments:

Post a Comment