Petr
aliyeokoa michomo mitatu ya penati toka kwa Bayrn Munich na kufanikisha kuipa
ubingwa wa Kombe la Ulaya timu yake ya Chelsea, amesaini mkataba wa miaka mine
na Chelsea.
Petr
Cech alijiunga na Chelsea mwaka 2004 ambako amecheza Mechi 369, ikiwa ni mechi
nyingi zaidi kuchezwa na mchezaji kutoka
nje ya Uingereza katika klabu hiyo.
Mechi hizo zimeshuhudia chesea ikishinda
vikombe katika mashindano manne tofauti yaani Ligi ya Uingereza (EPL) mara
tatu, Kombe la FA mara mara nne, Kombe la Carling mara mbili na Kombe la
mabingwa wa Ulaya mara moja.
Baada
ya kusaini mkataba Cech alisema anafuraha kubwa kuwa sehemu ya timu kubwa ya
Chelsea kwa miaka mingine minne huku akiamini kuwa miaka hiyo minned itakuwa ya
mafanikio kama ilvyokuwa miaka nane iliyopita.
Petr
Cech ametoa mchango mkubwa sana katika ushindi wa timu yake ya Chelsea kwenye
Kombe la FA na lile la mabingwa wa ulaya kwa kuokoa mikwaju mbalimbali golini
kwake ambayo ingesababusha madhara.
Atakubukwa
pia kwa kuokoa mkwaju wa penati wa Arjen Robben wa Bayern Munich katika
fainali ya Kombe la mabingea katika muda wa nyongeza na kuokoa peati mbili pia
wakati wa kipindi cha kupigiana mikwaju ya penati baada ya kumalizika kwa muda
wa nyongeza huku timu hizi zikiwa sare.
Mkurugenzi wa
timu ya Chelsea Ron Gourlay alisema kuwa anathamini mchango mkubwa wa Petr Cech
kaika kipindi hikik cha mafanikio makubwa kwa Chelsea na wamefurahi kuwa naye
tena katika kipindi hiki mpaka mwaka 2016.
No comments:
Post a Comment