WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Saturday, May 19, 2012

Drogbaaaaaaaaa… Ni Chelsea Mabingwa wa Ulaya



Kinyume cha matarajio ya wengi kwa kuzingatia takwimu za Bahati nasibu za mshindi, Chelsea FC imelichukua Kombe la mabingwa Ulaya nyumbani kwa wapinzani wao Bayern Munich. Ushindi ambao umeshuhudiwa na mmiliki wa Chelsea FC Roman Abramovich
Chelsea na Bayern Munich kabla ya Mechi

Nakshi iliwekwa uwanjani na mashabiki wa Bayern Munich ikisomeka JIJI LETU, UWANJA WETU, KOMBE LETU
Kwa Abramovich ushindi huu na kile alichokishuhudia pale  Allianz Arena ilikuwa kama ndoto kwani katika miaka yake tisa pale Stamford Bridge ameshawafukuza makocha nane na kuwasajili wachezaji 66 ambapo ametumia zaidi ya Paundi Bilioni Moja (£1billion). Hivyo hakuamini kuwa kikosi hiki cha muda mrefu kilichoanza kuishiwa Nguvu na Kocha wa Muda wangeweza kuleta kombe Stamford Bridge
Mchezo ulikuwa na mvutano tangu mwanzo mpaka mwisho huku wenyeji Bayern Munich wakimiliki mpira kwa kiasi kikubwa na kupata Kona nyingi 20 huku Chesea wakipata kona moja iliyozaa goli la kusawazisha.
Goli la kwanza la Bayern Munich  lililofungwa Kipindi cha pili dakika ya 83 lilipachikwa kimiani na Thomas Muller Na kufanya uwanja uzizime kwa shangwe, nderemo na vifijo na kupeleka simanzi kwa mashabiki wa Chelsea. Dakika tano baadaye kona ya kwanza  iliyopigwa na Juan Mata iliunganishwa kwa kichwa na mchezaji Didier Drogba (34) na kuzaa goli la kusawazisha. 
Drogba akishangilia goli alilofunga la kusawazisha
Goli hili kama lilivyokuwa lile la Bayern Munich lilipokelewa kwa Shangwe kuu na mmashabiki, wachezaji na viongozi wa Chelsea waliokuwa kwenye benchi la ufundi. Mpaka mpira unakwisha mabao yalikuwa 1 – 1 hivyo kusababisha mpira kuchezwa kwa muda wa nyongeza  wa dakika 30 ambao ulishuhudia magoli yakilala Njaa.
Mikwaju ya penati iliyofuata kwa mujibu wa kanuni ndio iliyoamua mshindi. Haikuwa rahisi kwa timu yoyote mpaka ulipopigwa mkwaju wa Mwisho wa penati ndipo mshindi alipatikana. Mkwaju wa mwisho wa penati uliokuwa ukisubiriwa ambao ulipigwa na Didier Drogba ndio ulioamua matokeo kwani mpaka ilipopigwa penati ya mwisho ya Bayern Munich mabao yalikuwa 3 -3 huku kila timu ikiwa imekosa penati moja. Hivyo Mchezo ukamalizika huku Chelsea wakitoka vifua mbele kwa ushindi wa  magoli 4- 3 kwenye Penati.
Kipa wa Chelsea akiokoa Penati iliyosababishwa na Didier Drogba 
wakati wa muda wa nyongeza

Matokeo haya yatabadilisha mtizamo, maamuzi na mikataba kwa timu, wachezaji, kocha na viongozi wa timu lakini jicho litatupwa zaidi kwa Roberto Di Mateo aliyeichukua na timu kutoka kwa kocha Andre Villas-Boas wakati ikichechemea na kufanikisha kupeleka makombe mawili Stamford Bridge. Aidha Didier Drogba ambaye mkataba wake unaokwisha msimu wa Joto ulikuwa umezungukwa na hisia za kutosainiwa tena lakini kwa matokeo haya Roman  Abramovich ndiye anayejua zaidi.
Goli la kusawazisha la Drogba
Baada ya kupokea kombe hili Drogba alilichukua na kumpelekea Roman Abramovich akiashiria kumuambia kuwa kazi uliyotutumaa tumemaliza.
Kazi uliyotutuma Tumemaliza....
Drogba akiondoka uwanjani



Drogba pia alikuwa mtu mweny Furaha sana kwa kuibuka shujaa na kupingana na kauli ya Kocha wa Bayern Munich Jupp Heynkes ambaye alipoulizwa kabla ya mechi kuhusu hofu ya kushindwa kutokana na Chelsea kuwa na washambuliaji mahiri kama Drogba: Jupp Heynkes alijibu na kusema kuwa Drogba ni muigizaji mahiri tu……

Tumeona leo uigizaji wa Drogba pale alipoipatia timu yake Goli la Kusawazisha kisha kuipatia ushindi Chelsea pale alipofunga penati ya Mwisho.
Mpira uliokwamishwa wavuni na mkwaju wa Penati ya Mwisho iliyopigwa na Drogba na kuamua mshindi wa Kombe la Maningwa wa Ulaya

Ushindi huu umesababisha mwanamuziki mashuhuri wa uingereza Jahmaal Noel Fyffe (Chipmunk)Kudiriki kusema kupitia ujumbe kwenye Mtandao wa Jamii Twitter kwamba “Drogba Ni Chelsea”

Hongera Chelsea

Hongera Di Mateo

Hongera Drogbaaaaa


No comments:

Post a Comment