WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Sunday, April 15, 2012


WASHINDI WA KILI MUSIC AWARDS 2012


Tunzo za Muziki za Kilimanjaro zijulikanazo zaidi kama “Kili Music Awards” Zilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City Usiku wa Jumamosi ya tarehe 14 Aprili 2012. Safu ya Wanamuziki waliowania tunzo mwaka huu 2012 ilitawaliwa na majina ya vijana wa kiume zaidi huku wakike  wakionekana zaidi kwenye vipengele vinavyohusika na jinsia yao.
Kwa Mujibu wa George Kavishe Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, mchakato wa kuwapata washindi wa tunzo za mwaka huu ulivuka lengo la idadi ya kura katika njia zote zilizotumika rasmi kwa makusudi hayo yaani ujumbe mfupi wa simu, vipeperushi, barua pepe na mitandao. Kuvukwa kwa lengo lililowekwa kunaashiria kukubalika na kupokelewa vema kwa tunzo hizi na Jamii. Kukamilika kwa shughuli hii ambako hatimaye kulipambwa na nderemo na vifijo pale Ukumbini Mlimani City Kulishuhudia tunzo hizi zikienda kwa wafuatao:

1)      Wimbo Bora Wa Raggae - -Arusha Gold Wa Warriors From East.

2)      Wimbo Bora Wa Dance Hall - Maneno Maneno Wa Queen Darlin.

3)      Wimbo Bora Wa Zouk Rhumba - Dushelele Wa Ali Kiba.

4)      4.Bora Wenye Vionjo Vya Kiasili - Vifuu Utundu Wa A.T

5)      Wimbo Bora Wa Taarabu - Nani Kama Mama Wa Mashauzi Classic ( Aisha Mashauzi).

6)      Wimbo Bora Wa Kiswahili - Dunia Daraja Wa Twanga Pepeta

7)      Wimbo Bora Wa Afro Pop - Hakunaga Wa Suma Lee

8)      Wimbo Bora Wa R&B - Number One Fan Wa Ben Paul

9)      Wimbo Bora Wa Hip Hop - Mathematics Wa Roma

10)  Msanii Bora Anaechipukia  Ommy Dimpoz (Nai Nai Singer).

11)  Rapa Bora Wa Band -Kalijo Kitokololo

12)  Msanii Bora Wa Hip Hop - Roma Mkatoliki

13)  Wimbo Bora Wa Kushirikishwa - Nai Nai Wa Ommy Dimpoz Ft. Ali Kiba

14)  Wimbo Bora Wa Afrika Mashariki - Kigeugeu Wa Jaguar

15)  Mtumbwizaji Bora Wa Kike - Khadija Kopa

16)  Mtunzi Bora Wa Mwaka - Diamond

17)  Mtumbwizaji Bora Wa Kiume - Diamond

18)  Mtayarishaji Bora Wa Mapigo Ya Muziki - Maneke

19)  Video Bora Ya Mwaka - Mawazo Wa Diamond

20)  Wimbo Bora Wa Mwaka - Hakunaga Wa Suma Lee

21)  Hall Of Fame - Taasisi JKT

22)  Hall Of Fame Kwa Mtu Binafsi - King Kikii

23)  Hall Of Fame Kwa Mtu Binafsi - Dr. Remmy Ongala

24)   Mwimbaji Bora Wa Kike - Lady Jay Dee

25)  Mwimbaji Bora Wa Kiume - Barnaba
Hongera waandaaji wa Kili Music Awards 2012 , Mlitupa Burudani na kuendelea kutuibulia Vipaji – Kudoz All!

No comments:

Post a Comment