WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Monday, April 16, 2012


FABRICE MUAMBA ATOKA HOSPITALI

Kwenye Picha hapo juu Muamba anaonekana akiwa na Madaktari wa hospitali alikolazwa Barts Health NHS Trust Dr Andrew Deaner na Dr Sam Mohiddin

Hatimaye kiungo wa timu ya Bolton ambaye alianguka ghafla uwanjani tarehe 17 Machi 2012 ameruhusiwa kutoka hospitali leo. Muamba alionekana mwenye afya na Furaha wakati akitoka hospitali na kuwashukuru wote waliohusika katika kumhudumia wakati wote alipokuwa hospitali.

Aidha aliwasifu Barts Health NHS Trust kwa moyo wa kujitolea, uweledi na utaalamu wao katika kipindi chote alichokuwa anapata matibabu. Aidha aliwashukuru wasamaria wema wote kwa salamu na dua zao za kumtakia heri.

Baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali Muamba atatumia muda huu akiwa na familia yake akiendelea kupata nafuu

No comments:

Post a Comment