WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Wednesday, April 25, 2012

WACHEZAJI PUNGUFU WA CHELSEA WAIPELEKA CHELSEA FAINALI
Goli la Fernando Torresi la dakika ya 90 lilipeleka kilio Nou Camp kwa vijana wa Pep Guardiola katika mchezo wa marudiano kati ya Chelsea na Barcelona. Huku wakicheza Pungufu kuanzia dakika ya 37 ambapo Mchezaji wa the Blues John Terry alipewa kadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya Alexis Sanchez, vijana wa Chelsea walipambana kishujaa mpaka kopenga cha mwisho kilipopulizwa na Mwamuzi wa kimataifa mturuki Cuneyt Cakir. Kadi hii ilitolewa huku Barcelona ikiwa inaongoza kwa goli 1-0, goli lililofungwa dakika ya 35 na Sergio Besquests
Kuanzia Dakika ya 37 Chelsea waliendelea kucheza wakiwa Pungufu na kukabiliana na wachezaji machachari na weledi wa kikosi cha Barcelona ambao walikuwa kwenye uwanja wa Nyumbani, Nou Camp.
Goli lapili kwa Barcelona liliofungwa na Andrea katika dakika ya 44 liliwafanya Barcelona kuongoza kwa magoli 2 – 0 na kupeleka matumaini makubwa ya Ushindi kwa kuzingatia matokeo yao ya awali na Chelsea kule Stamford Bridge.
Nderemo na vifijo kuchagiza ushindi zaidi kutoka kwa mashabiki wa Barcelona waliohudhuria mechi hii zilififia kwa Muda katika dakika ya 49 ambapo Ramires aliipatia Chelsea goli la Kwanza na kufanya matokeo yawe 2-1.
Goli hili lilifufua matumaini kwa vijana wa Chelsea ambao wamekuwa na kipindi kigumu katika msimu huu kwenye ligi ya nyumbani hivyo kuwemo kwenye mashindano haya na hatua waliyoifikia iliwapa matumaini mapya. Matumaini haya yalipandisha mori na shamrashamra za mashabiki wa Chelsea waliokuwepo uwanjani hapo wakishuhudia mechi kati ya timu hizi mbili. Hivyo mpaka wanakwenda kwenye Mapumziko Barcelona walikuwa wanaongoza kwa Magoli 2 – 1

Mashabiki wa Chelsea wakiwachagiza na kushangilia timu yao Uwanjani, Nou Camp
Katika dakika ya 49 Barcelona ilipata Penati ambayo ilipigwa na Lionel Messi, mkwaju ambao uligonga mwamba na kuikosesha Barcelona kupata goli la tatu. Kukosa Penati hii kunamfanya Messi kushindwa kupata goli katika Mechi nane mfullulizo walizocheza na Chelsea
Mabadiliko yaliyofanyika kipindi cha pili kwenye timu ya Chelsea na kumuingiza Fernando Torres yalipeleka kilio Nou Camp katika dakika ya 90 ambapo Fernando Tores aliifungia timu yake ya Chelsea goli la kusawazisha. Mpaka Mpira unakwisha matokeo yalikuwa 2-2 na ukifanya majumuisho ya Mechi zote mbili unapata Jumla ya Magoli 3 kwa Chelsea na 2 kwa Barcelona. Matokeo ya Mechi hii yanaifanya Chelsea iwe imecheza michezo minne katika uwanja wa nyumbani wa Barcelona Camp Nou bila kufungwana Barcelona. Katka mechi hizo zote matokeo yalikuwa ni sare. Matokeo haya yalishangiliwa sana na mashabiki na wachezaji wa Chelsea kwa imitindo mbalimbali
Fernando Torres akishangilia bao lake alilolifunga dakika ya 90
Shangwe kwa wachezaji wa Chelsea baada ya Ushindi
Drogba akishangilia Ushindi wa Chelsea
Branislav Ivanovic akishangilia Ushindi wa Chelsea

Kwa matokeo haya Barcelona inakuwa imetolewa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ubingwa wa mashindano haya. Aidha John Terry aliomba msamaha kwa wachezaji wenzake na mashabiki wa Chelsea kutokana na kosa alilolifanya na kumsababishia Kadi Nyekundu kwenye Pambano lile ambalo lilihitaji kila aina ya msaada kuihakikisha ushindi timu yake.
Mshindi wa Mchezzo wa leo kati ya Real Madrid na Bayern Munich ndio utakaoamua timu itakayokutana na Chelsea


No comments:

Post a Comment