WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Wednesday, April 25, 2012

NI BAYERN MUNICH NA CHELSEA FAINALI ZA KOMBE LA MABINGWA

NI BAYERN MUNICH NA CHELSEA FAINALI ZA KOMBE LA MABINGWA
Matokeo ya Mechi ya jana ambayo ilizikutanisha timu Mbili real Madrid na Bayern Munich katika mchezo wa marudiano pale Estadio Santiago Bernabeu, Madrid yaliitoa Real Madrid nje ya kinyang’anyiro cha ubingwa wa Kombe la mabingwa baada ya mikwaju ya Penati. Mechi hii ilikuwa ya marudiano baada ya ile mechi ya kwanza iliyofanyika uwanja wa nyumbani wa Bayern Munich Allianz Arena, Bayern kumalizika kwa Bayern Munich kuifunga Real Madrid magoli 2-1.
Furaha ya Ushindi - Wachezaji wa Bayern Munich
Goli la dakika ya 6 la mkwaju wa Penati lililofungwa na Chrisian Ronaldo liliwafanya wenyeji Real Madrid kupata ari zaidi ya ushindi kutokana na ukweli kwamba goli hilo lilikuwa linafanya matokeo yao ya jumla yawe sare, hivyo kuifanya iongeze Nguvu ya kutafuta ushindi kuweza kufuzu kuingia katika fainali ya Ligi hii ya mabingwa.
Pasi ya dakika ya 14 kutoka kwa Mesut Oezel ilimkuta Christian Ronald akiwa peke yake na hivyo kupiga shuti lililompita mlinda mlango wa Bayern Munic Manuel Neuer na kuwapa Real Madrid goli la Pili. Bao hili lilifanya  Real Madrid iongeze katika mchezo na pia katika jumla ya magoli ya mechi mbili. Nyimbo za furaha na ushangiliaji kutoka kwa mashabiki wa Real Madrid zilizidi kuongezeka kufurahia ushindi

Furaha ya washabiki wa Real Madrid iliingia doa dakika 13 baadaye kutokana na Bayern Munich kupata bao la kwanza. Bao la Arjen Robben wa Bayern Munich katika dakika ya 27 lilichochea ulinzi na mashambulizi zaidi kutoka kwa Bayern Munich ambao walikuwa na nia kubwa ya kuona wakiingia fainali ukizingitatia ukweli kuwa Fainali za kombe la Mabingwa Msimu huu zimepangwa kufanyika Mjini Munich Ujerumani ambako ni nyumbani kwa timu ya Bayern Munich.Watazamaji walishuhudia kandanda safi lenye ushindani katika kipindi cha kwanza  ambacho likimalizika kwa mabao 2 kwa Real Madrid na 1 kwa Bayern Munich

Patashika, Piga nikupige, Juhudi na hekaheka za kuwania ushindi kwa wachezaji wa Bayern Munich na wale wa Real Madrid zilitawala katika Mchezo huu
Hatimaye Ushindi ni dhahiri kwa Bayern Munich

Real Madrid walikuwa na nafasi kubwa ya kushinda baada ya kutengeza nafasi nyingi za kufunga na kufanikiwa kupata magoli mawili tu. Mchezaji wa safu ya mashambulizi Sami Khedira alishindwa kufunga katika dakika ya tatu baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Angel Di Maria. Lakini mnamo dakika ya 6 Real Madrid walipata penati baada ya Mpira uliopigwa na Angel Di Maria kumgonga mkononi David Alaba.
Bayern walipata nafasi mbili ambapo Robben alishindwa kutumia nafasi iliyotengenezwa na David Alaba na pale ambapo Franck Ribery aliposhindwa kumalizia mpira uliotokana na mkwaju wa Mario Gomez baada ya kuzuiwa na Mchezaji wa Real Madrid Khedira

Kipindi cha pili kilishuhudia timu hizi zikimaliza dakika 45 bila kufungana na hivyo kulazimisha muda wa ziada kwa mujibu wa taratibu. Mpaka kipenga cha mwisho cha muda wa ziada kinapulizwa matokeo yalikuwa  Real Madrid 2 Bayern Munich 1 kwa matokeo haya jumla ya magoli kwa mechi zote mbili ikiwa 3-3. Ili kumpata mshindi, timu hizi ziliingia katika kipindi cha mikwaju ya penati ambapo Bayern Munich ilifanikiwa kunasisha wavuni mikwaju 3 dhidi ya mkwaju 1 Ulionasihshwa wavuni na Real Madrid.
Mlinda mlango makini wa Bayern Munich Manuel Neuer alifanikiwa kuokoa mikwaju ya Penati ya Ronaldo na Kaka wakati mkwaju wa Sergio Ramos ukipaa juu ya goli na kufanya mkwaju pekee wa  Bastian Schweinsteiger kujaa kimiani. Hii ni mara ya Pili kwa mashindano makubwa kama haya kushuhudia mfungaji mahiri Christiano Ronaldo akikosa Penati baada ya kukosa penati kwa mtindo huo mwaka 2008 kwenye fainali dhidi ya Chelsea alipokuwa akiichezea Manchester United

Cristiano Ronaldo baada ya Kukosa Penati

Kwa upande wa Bayern Munic, wachezaji, Mario Gomez, David Alaba na Bastian Scheinsteiger ndio walioizamisha mikwaju ya Penati wavuni.
Bastian akionyesha furaha yake baada ya kufunga mkwaju wa penati na kulizamisha kabisa Jahazi la Real Madrid


Mpira ulimalizika na kuwaacha vijana wa Jupp Heynckes wakitoka uwanjani kifua mbele kwa magoli 3 -1 ya mikwaju ya penati na kufuzu kuingia fainali na Chelsea mapema mwezi ujao.
Kwa matokeo haya Bayern Munich inasonga mbele katika kuwania ubingwa katika fainali itakapopambana na Chelsea katika uwanja wake wa nyumbani Pale Munich, Ujerumani Jumamosi, tarehe 19 Mei 2012

Mchezo huu ulishuhudia kadi saba za njano ambazo ziliwaendea wachezaji wanne wa Bayern Munich na wachezaji watatu wa Real Madrid na hivyo kuathiri timu zao katika fainali.
Bayern Munich italazimika kucheza bila wachezaji wafuatao itakapopamba na Chelsea kwenye fainali, David Alaba, Holger Badstuber and Luiz Gustavo. Vile vile Chelsea ambayo itapambana na Bayern Munich itawakosa wachezaji wake muhimu kama Ramires, John Terry, Branislav Ivanovic na Raul Meireles kutokana na kupewa kadi katika mchezo wake wa Nusu fainali na Barcelona.

Kwa mchezo huu wa fainali dhidi ya Chelsea, Bayern Munich itakuwa ni mechi yake ya tisa ya fainali za kombe la mabingwa wakati Chelsea itakuwa ni mechi yake ya pili ya fainali. Katika fainali hizo Bayern Munich imeshinda mara nne wakati Chelsea haijawahi kushinda


No comments:

Post a Comment