WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Tuesday, April 24, 2012

ROBIN VAN PERSIE ACHAGULIWA KUWA MCHEZAJO BORA WA MWAKA
Robin Van Persie

Mtikisa Nyavui mahiri wa Arsenal, Robin Van Persie amechaguliwa kuwa Mchezaji bora wa Mwaka na Muungano wa Waandishi wa Mpira wa Miguu Uingereza (Football Writers Association). Muungano wa waandishi wa magazeti na wale wa kujitegemea wa Habari za Mpira wa Miguu ulianzishwa mwaka 1947 ukiwahusisha waandishi wa habari za mchezo wa mpira wa miguu Uingereza. Kila mwaka Muungano huu wa wandishi huwa unatoa Tunzo kwa Mchezaji bora wa mwaka ambaye ametoa mchango mkuwa kwenye mchezo wa mpira wa miguu. Tunzo hii ni kati ya tunzo kuu mbili zinazoheshimika sana katika Soka la Uingereza; tunzo nyingine ni ile inayotolewa na Muungano wa wachezaji wa Kulipwa wa Mpira wa miguu (Professional Footballers Association) yaani Tunzo ya Mchezaji bora wa Mwaka ya PFA. Tunzo hii imeanza kutolewa rasmi kwenye msimu wa 1973/4

Ushindi wa kishindo wa Van Persie katika tunzo iliyotolewa na FWA umetokana na kura takribani 400 za waandishi wa habari matokeo ambayo yamemuacha nyuma Mtikisa nyavu wa Manchester United Wayne Rooney. Aliyefuata katika kura hizo ni mchezaji wa Manchester United Paul Scholes huku nafasi ya nne ikikamatwa na Mchezaji wa Fulham Clint Dempsey.

 Hii inakuwa Tunzo ya pili mfululizo ndani ya Siku tatu kwa Van persie baada ya kushinda tunzo ya Mchezaji bora wa Mwaka wa wachezaji wa Kulipwa iliyotolewa na Professional Footballers Association. Tunzo hii ya PFA inamaanisha kuwa Robin Van Persie ameweza kunyakua tunzo zote mbili za juu za zinazoheshimika katika mpira wa miguu Uingereza.

Tunzo hizo mbili kwa mpigo zinamfanya Van Persie kuwa mchezaji wa 16 kuchukua tunzo mbili kwa wakati mmoja. Mchezaji wa mwisho kupata tunzo hizo kwa mpigo alikuwa Wayne Rooney mwaka 2010

Van Persie amefunga Jumla ya Magoli 34 katika mashindano yote yakiwamo 27 katika ligi

Video Clip hapo chini inamuonesha Robin Van Persie akifunga goli katika Mechi dhidi ya Everton

No comments:

Post a Comment