HATIMAYE
BINGU WA MUTHARIKA AZIKWA “TAJ MAHAL”
Marehemu Bingu wa Mutharika (1934 - 2012)
Bingu
wa Mutharika (78) aliyefariki tarehe 5 Aprili 2012 kwa ugonjwa wa Moyo, Hatimaye
amezikwa “Maphumulo wa Bata,” jina la lugha ya kichewa linalomaanisha Pumziko la Amani, Sehemu ambayo imekuwa pia ikiitwa Taj Mahal. “Maphumulo wa Bata,” imejengwa
kwenye Shamba binafsi la marehemu Bingu wa Mutharika huko Ndata
Maphumulo wa Bata ambapo pia hujulikana kama Taj Mahal
Taj Mahal Halisi iliyoko Agra, India iliyojengwa na Mtawala Shah Jahan
“Maphumulo wa Bata,”
umepewa jina la Taj Mahal kutokana na ukubwa wake na ueledi uliotumika kati
Usanifu wa ujenzi wake na gharama kubwa iliyotumika katika Ujenzi wake. “Maphumulo
wa Bata,” ilijengwa na Marehemu Bingu wa Mutharika kwa ajili ya Maziko ya mke
wake Ethel Bingu wa Mutharika aliye fariki mwaka 2007. Kama ilivyokuwa kwa
Mtawala Shah Jahan, Bingu wa Mutharika naye amepumzishwa “Maphumulo wa Bata,” au
Taj Mahal kama inavyojulikana huko Malawi. Bingu wa Mutharika alitaka eneo hilo
kuwa Mnara wa taifa ambao utatembelewa na wamalawi kama sehemu ya Makumbusho ya
Taifa. Ni katika Shamba hilo pia ambako Bingu wa Mutharika alijenga Kasri kubwa
yaKifahari ambayo ililalamikiwa sana na wananchi wa Malawi wakati wa Ujenzi
wake wakihusisha ujenzi huo na ubadhirifu mkubwa wa Fedha za Malawi mara baada
ya Kuchaguliwa kuwa Raisi mwaka 2004
Kasri ya Bingu wa Mutharika iliyojengwa kwenye Shamba lake Ndata
Bingu wa Mutharika, Mwanasiasa na Mchumi
alichaguliwa kuwa raisi wa tatu wa Malawi kwa mara ya kwanza Mwezi Mei, 2004 na
aliendelea kuwa Raisi mpaka alipofariki. Bingu wa Mutharika alikuwa pia Raisi
wa Democratic Progressive Party ambayo ndio ina wabunge wengi zaidi bungeni
baada ya Uchaguzi mkuu wa Mwaka 2009.
Mazishi ya Bingu wa Mutharika yamehudhuriwa
na watu mbalimbali mashuhuri wakiwemo Maraisi kadha wa Afrika kama Robert
Mugabe wa Zimbawe, Mwai Kibaki wa Kenya, Armando Guebuza wa Msumbiji,
Hipikefunye Pohamba wa Namibia na Jakaya Kikwete wa Tanzania ambao pia
walihudhuria ibada ya Mazishi mjini Blantyre, Malawi.
Gharama za mazishi ni kiasi cha kwacha
milioni 242 ambazo ni sawa na Dola za Marekani Milioni Moja na nusu (US $ 1.5m)
Kwa heri Bingu wa Mutharika, Kwa heri Raisi wa Tatu wa Malawi
No comments:
Post a Comment