WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Friday, April 27, 2012

KWA HERI PEP GUARDIOLA....


Mazungumzo marefu kati ya Kocha wa Barcelona, Pep Guardiola leo Jumanne 27 Aprili 2012 na Raisi wa timu Sandro Rosell  yaliishia katika tamko rasmi la Pep kutosaini mkataba mwingine na Bracelona. Hatua hi inakuja baada ya kushuhudia Barcelona ikiondolewa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ushindi katika kombe la mabingwa dhidi ya Chelsea.
Kabla ya kutangaza uamuzi huu, Guadiola aliongea na wachezaj wake wakati wa Mazoezi asubuhi ya leo kuhusu uamuzi wake wa kutosaini mkataba mwingine wa kukinoa kikosi cha Barcelona. Guardiola anaondoka Nou Camp baada ya miaka minne ya mafanikio kama Kocha wa Barcelona. Guardiola alanza kukifundisha kikosi cha kwanza cha Barcelona akitokea Barca B mwaka 2008; hatua ilyomfanya awe kocha mwenye mafanikio zaidi katika historia ya Barca.

Guardiola aliiongoza Barcelona kuchukua ushindi marambili kwenye ligi ya mabingwa, makombe matatu La liga, ushindi mara moja kwenye Copa del rey, makombe matatu kwenye supercopas, Makombe mawili ya UEFA super Cups na makombe mawili ya Fifa Club world Cups. Anaondoka Nou Camp akiwa amefanikisha ushindi wa makombe 13 Barcelona katika miaka minne.
Pep Guardiola akiwa ameshika kombe la Mabingwa Mei 2011 baada ya kuifunga Manchester United, Wembley Stadium

Hata hivyo kutolewa na Chelsea kwenye kinyang’anyiro cha ubingwa wa kombe la mabingwa kulikuja siku tatu baada ya kufungwa na wapinzani wao wakubwa Real Madrid kwenye uwanja wa nyumbani na kupeperusha matumaini ya kunyakua ubingwa wa ligi ya nyumban (Primera Division Crown). Kipigo hiki cha Real Madrid kiliweka tofauti ya pointi saba baina ya timu hizi mbili huku wakiwa wamebakiwa na michezo minne mkononi
Guardiola amekishikilia kikosi cha Barcelona ka kusimamia maendelo ya timu na wachezaji wake akishuhudia Loinel Messi akiwa mchezaji bora wa mwaka mara tatu na kuimarisha kiwango cha wachezaji kama Xavi na Iniesta. Mafanikio na majina ya wachezaji haya yamekuwa yakibeba usanifu wake.
Raisi wa Barcelona Sandro Rosell
Raisi, Rosell ametoa shukrani zake za dhati kwa Pep Guardiola kwa Furaha ambayo ameipatia Barcelona kipindi chote cha utumishi wake.
Siku zote Guardiola amekuwa akisisitiza kufanya chochote ambacho ni bora kwa Barcelona hivyo wakati wa mazungumzo marefu na Raisi wa Klabu, Guardiola aliendelea kusisitiza msimamo wake wa kutoendelea kuifundisha klabu yake akiamini hicho ndicho kitu bora kwa klabu.
Kwa heri Guardiola!

No comments:

Post a Comment