WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Sunday, April 22, 2012

MUAMBA AZUNGUMZIA KILICHOTOKEA 17 MACHI 2012

F

abrice Muamba ameongea kwa mara ya kwanza kuhusu tukio la kutisha alipoanguka kiwanjani dakika ya 41 wakati timu yake ya Bolton ikicheza na Tottenham tarehe 17 Machi 2012. Kitaalamu kuanguka na kupoteza fahamu kwa Muamba kulitafsiriwa kama Kifo cha dakika 78. Iliwachukua madaktari Mistuo ya Moyo mitatu (defibrillator shocks) kuufanya moyo wa Muamba uanze kufanya kazi tena. Alifanyiwa mishtuko hiyo mara mbili kiwanjani na mmoja akiwa kwenye gari la wagonjwa kueleka Hospitali.

“Nilikuwa nakimbia, nikasikia kizunguzungu, nikawa sioni ...kisha nikajihisi nikianguka”

“...Nilikuwa nakimbia kuifuata pasi iliyopigwa na Martin Petrov kwa kiungo chetu cha kushoto na nilipokuwa narudi kati nikahisi kizunguzungu kidogo.. hakikuwa kizunguzungu cha kawaida, nilikuwa kama nakimbia kwenye mwili wa mtu mwingine, nikaendelea kukimbia, nikahisi tena kizunguzungu macho yakapoteza nuru- sikuwa na maumivu yoyote wala mguso wowote kifuani. Nikaanza kuona vitu viwili viwili. Nilihisi kama ndoto. Hakukuwa na yoyote karibu yangu nilipohisi kuanguka.

Kitu cha mwisho ninachokumbuka ni sauti ya Dedryck Boyata (Mchezaji wetu katika safu ya Ulinzi) akiniambia kwa sauti nirudi nyuma na kusaidia safu ya ulinzi. Nilijihisi nikianguka na kuhisi vishindo viwili kichwa changu kilipogonga ardhini. Giza, hakukuwa na kitu, nilikuwa mfu”.
Wachezaji wakiwa na Simanzi baada ya Muamba Kuanguka na kupoteza fahamu uwanjani


Muamba anategemea kuwepo uwanjani tarehe 2 Mei kushuhudia mpambano wakati timu yake ya Bolton itakapopambana na Tottenham ikiwa ni marudio ya mechi iliyoahirishwa siku alipoanguka uwanjani.
Muamba anakumbuka kuwa kabla ya Mechi ile aliomba ulinzi wa Mungu. Alisema Mungu alikuwa pamoja naye kwani kilichotokea ni zaidi ya muujiza.
“Siku ya Mechi nilisali na Baba yangu kumuomba mungu anilinde na Mungu hakuniangusha. Ninatembea kwa ushuhuda wa nguvu za Maombi. Kwa dakika 78 nilikuwa mfu na kama ningeishi ningepata madhara makubwa kwenye ubongo. Lakini mimi ni mzima sana nimekaa na ninaongea. Mungu alikuwa ananiangalia na kunilinda”
Muamba amewekea Kifaa kwenye kifua cha kuzuia (efibrillator) shambulio kama hilo endapo litatokea. Kwa sasa Muamba anaangaliwa kwa ukaribu na timu imesema wazi kuwa endapo Muamba atapenda kuhudhuria mechi ya Bolton itategemea zaidi hali yake ya kiafya

No comments:

Post a Comment