WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Sunday, April 22, 2012

Kwa Nini El-Clasico?


El Clásico ambayo hujulikana pia kama El Derbi Espanol ni jina linolotumiwa wanapokutana mafahari wawili wa Soka wa Hispania yaani Real Madrid na FC Barelona. Katika ligi, timu hizi hukutana mara mbili kwa mwaka au hukutana tena endapo timu hizi zitakutana katika mashindano mengine kama UEFA. Timu hizi ndizo zinavuta mashabiki, wafuatiliaji na watazamaji wengi zaidi duniani zinapokutana ukiacha mashindano ya UEFA. Ushindani huu unaovuta hisia za watazamaji na wafuatiliaji wengi unatokana mafanikio ya timu hizi katika Soka, utajiri, na ukubwa wa miji zinatokea timu hizi yaani Madrid na Barelona. Real Madrid haijawahi kushuka daraja tangu ilipoanzishwa.

Wakati mwingine ushindani huu wa soka baina ya timu hizi mbili umehusishwa mpaka kwenye nyanja za siasa za Hispania ambapo Real Madrid inahusishwa na hama cha Spanish Nationalism wakati Barcelona inahusishwa na Calatan Nationalism. Ushindani wa timu hizi ndioo unaoaminika kuwa mkubwa zaidi katika ulimwenu wa soka Duniani. Na hii ndio inavuta hisia za watu wengi zaidi ulimwenguni


CHRISTIANO RONALDO AIZAMISHA BARCELONA NYUMBANI NOU CAMP

Goli la dakika ya 73 kipindi cha pili la Christiano Ronaldo (27) liliihakikishia Real Madrid Ushindi ambao uliipadisha Real Madrid kwa tofauti ya Pointi saba (7) Mbele ya Washindani wao wakubwa Barcelona. Ushindi huu ulipatikana nyumbani kwa timu hiyo bora duniani Barcelona pale Nou Camp Jumamosi ya Tarehe 22 Aprili 2012.

Timu zote mbili zilikuwa zimetoka katika mechi za UEFA ambapo zote zilipoteza katika round hiyo; Mechi hizo zilishuhudia Barcelona ikifungwa Bao Moja na Chelsea Jumatano tarehe 18 Aprili 2012 pale Stamford Bridge na Real Madrid ilifungwa 2 – 1 na Bayern Munich Jumanne tarehe 17 April 2012, Muuaji wa Real Madrid akiwa Mario Gomez ambaye aliupeleka mpira Kimiani na kupata goli la Pili katika dakika ya 90
Kwa ushindi huo, Real Madrid imesafisha njia kueleka kwenye Ubingwa wa Ligi ya Hispania







No comments:

Post a Comment