WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Saturday, April 28, 2012

BARCELONA: KOCHA MPYA BAADA YA GUARDIOLA

Kupatikana kwa jina la mrithi wa Guardiola, Tito Vilanova (42) mara tu baada ya kutangazwa kuondoka kwa Guardiola kwenye mkutano wa waandidhi wa habari kulishangaza wengi. Awali kulipokuwa na tetesi za Guardiola kutotia saini mkataba mwingine, majina ya makocha maarufu yalikuwa yakitajwa tajwa na wadau mbalimbali; majina kama Ernesto Valverde, Laurent Blanc na Marcelo Bielsa
Kocha Mteule Tito Vilanova (42)
Akitangaza jina la kocha mpya, Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Andoni Zubizarreta alisema kuwa ni utaratibu wa Barcelona kuwa siku zote wanaposaka wachezaji huwa wanaanza kuangalia ndani ya timu yao kwanza kisha wanatafuta nje. Hivyo aliyekuwepo na kuweza kumudu nafasi hiyo ni Tito Vilanova.

Aliendelea kusema kuwa Tito Vilanova anawakilisha aina yao ya mchezo na mawazo yao na kwamba hakuna kocha mwingine kutoka nje ya timu ambaye angeweza kufanya hivyo. Ni wazi kuwa Tito yuko tofauti na Guardiola lakini atafanya kazi katika mtazamo ule ule.
Tito Vilanova aliwahi kuwa mchezaji wa kiungo wa Barcelona ambapo alicheza michezo 26 ya ya ligi ya hispania (La Liga). Alichaguliwa kuwa msaidizi wa Kocha wa Barcelona B mwaka 2007 chini ya Guardiola. Baada ya kuonyesha mafanikio katika kikosi hicho wote wawili Tito na Guardiola walipandishwa daraja na kuanza kukifundisha kikosi cha kwanza cha Barcelona mwaka 2008.
 Tito Vilanova na Pep Guardiola
Titio Vilanova anakumbukwa sana hadi leo kutoka na tukio la mwezi Agosti 2011 ambapo Kocha wa Real Madrid Jose Maurinho alipomvamia na kumkwaruza kwenye jicho baada ya ushindi wa timu anayoifundisha ya Barcelona kutwaa ubingwa  wa Super Cup – Hispania
Jose Maurinho akimsukuma Tito Vlanova kwa kumpelekea kidole kwenye jicho

TITO VILANOVA NI NANI?

·        Alizaliwa tarehe 17 Septemba, 1969 Bellcaire d'Emporda Girona, mji unaopatikana Gerona, Cataluna,  huko Hispania

·        Mwaka 1988 akiwa na Pep Guardiola alijiunga na Barcelona B ambapo alicheza kwa miaka miwili

·        Mwaka 1990 alicheza:lower-league Figueres.

·       Mwaka 1992:alihamia Primera Division Celta Vigo lakini hakupata nafasi katika kikosi cha kwanza

·       Mwaka 1995 aliondoka Celta na kuchezea ligi mbali mbali kati ya mwaka 1995 mpaka 2002 akiwa na timu kama:

o   Club Deportivo Badajoz

o   Real Club Deportivo Mallorca,

o   Unió Esportiva Lleida

o   Elche Club de Fútbol

·       Mwaka 2002 alistaafu kucheza soka akiwa katika timu ya Unión Deportiva Atlético Gramenet Milán (Gramenet)

·      Baada ya kustaafu soka aliendelea kuwepo katika fani ya soka mpaka alipofikia kuwa Mkurugenzi wa ufundi Tarrasa, timu ambayo uwanja waake wa nyumbani Estadi Olímpic de Terrassa, una uwezo wa kuchukua watazamaji 11.500. Aliondoka Terrassa akiiacha timu hii katika nafasi ya 6 katika ligi ya Segunda Division B

·      Mwaka 2007 alijiunga na Barcelona B kama msaidizi wa Kocha Pep Guardiola ambapo waliisadia timu kupanda daraja kwenda Segunda Division B.

·       Mwaka 2008 Tito alipandishwa daraja kuwa msaidizi wa kocha Pep Guardiola katika Kikosi cha Kwanza cha Barcelona. Makocha hawa wawili walileta mafanikio makubwa katika kikosi hiki cha kwanza kwa ushindi wa vikombe mbalimbali kwenye ligi ya ndani, ligi ya Ulaya na klabu bingwa ya dunia

·         Tarehe 27 Aprili 2012 Tito Vilanova anateuliwa kuwa Kocha wa kikosi cha kwanza cha Barcelona kuanzia msimu ujao kufuatia kuondoka kwa Kocha Mkuu Pep Giuardiola ambaye alisema kuwa hakuwa na nguvu tena za kuongoza timu na kupata zaidi kutoka kwa wachezaji kwenye kila mchezo. Pep alisema anahitaji kupumzika baada ya mchango wake wa miaka minne katika timu.

Baada ya kutangazwa jina la Tito Vilanova kama kocha mkuu wa wa Barcelona kwa kikosi cha kwanza, Pep Guardiola alionyesha kuridhishwa na uteuzi huo. Pep alisema kuwa klabu imefanya uamuzi bora kwa maendeleo ya tmu kwa vile anaamini kuwa Tito Vivanola ana uwezo mkubwa na wachezaji wanamjua vema. Anajua kuwa Tito atafanya mabadiliko machache na kuwapa wachezaji na klabu kile ambacho yeye asingeweza kuwapa kwa wakati huu.
Pep Guardiola kwenye mkutano na waandishi wa habari
Wakati haya yote yanaendelea, Lionel Messi hakuwepo kwa vile hakupenda kushuhuda tukio hili. Alisema Anamshukuru sana Pep Guardiola kwa vile ndiye aliyemfikisha hapo alipo na kumuwezesha kutwaa mataji mbalimbali kutokana na kupanda kwa kiwango chake. Aliamua kutohudhuria katika mkutano huo wa waandishi wa habari kwa vile anaamini watu wangependa kuona huzuni katika nyuso za wachezaji, kitu ambacho yeye asingependa kukionyesha
Messi akikumbatiana na Pep Guardiola baada ya kuwaarifu juu ya uamuzi wake mazoezini

Pep Guardiola akiaga baada ya mkutano wa waandishi wa habari
Tito Vilanova - Pamoja!


No comments:

Post a Comment