Matokeo ya Mechi ya Jumapili tarehe 12 November 2012
baina ya Yanga na Coastal Union pale Mkwakwani yalim-bainisha kiongozi wa ligi hiyo katika mzunguko wa kwanza huku mechi chache zikibaki kukamilisha mzunguko huo
Tumeshuhudia mengi katika Mzunguko huu wa
Kwanza; harakati, mikakati na juhudi mbalimbali kujiimarisha katika msimamo wa
Ligi. Harakati hizo zimeshuhudia Furaha na Amani hali kadhalika huzuni na
ghadhabukwa upande mwingine katika vilabu vya soka vinavyoshiriki ligi hii.
Lakini kama wasemavyo wengi, Soka ni mchezo wa Makosa! Makosa yako wewe huwa
nafasi kwa mpinzani wako endapo atayatumia Vema kama tulivyoona kwenye michezo
mbalimbali katika mzunguko huu.
Kuna mengi tumeyaona yanayohusisha Vilabu,
Kamati ya Ligi, Wadhamini, Wanachama, viongozi na wadau wote wa soka. Basi
kipindi hiki cha mapumziko kitakuwa kipindi muafaka kutathmini yote
yaliyojitokeza ili tuweze kuifanya ligi na mashindano haya kuwa Bora zaidi.
Msimamo mpaka mwisho wa ligi hii ulikuwa
hivi:
Nafasi
|
Timu
|
MP
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
+/-
|
Pts
|
1
|
Young Africans
|
13
|
9
|
2
|
2
|
25
|
10
|
15
|
29
|
2
|
Azam
|
13
|
7
|
3
|
3
|
17
|
11
|
6
|
24
|
3
|
Simba SC
|
13
|
6
|
5
|
2
|
20
|
11
|
9
|
23
|
4
|
Mtibwa Sugar
|
13
|
6
|
4
|
3
|
18
|
12
|
6
|
22
|
5
|
Coastal Union
|
13
|
6
|
4
|
3
|
16
|
14
|
2
|
22
|
6
|
Kagera Sugar
|
13
|
5
|
6
|
2
|
15
|
10
|
5
|
21
|
7
|
Ruvu Shooting
|
12
|
5
|
2
|
5
|
17
|
17
|
0
|
17
|
8
|
JKT Ruvu
|
13
|
4
|
3
|
6
|
13
|
20
|
-7
|
15
|
9
|
Tanzania Prisons
|
11
|
3
|
5
|
3
|
8
|
9
|
-1
|
14
|
10
|
JKT Oljoro
|
13
|
3
|
5
|
5
|
13
|
16
|
-3
|
14
|
11
|
Mgambo JKT
|
12
|
4
|
2
|
6
|
9
|
13
|
-4
|
14
|
12
|
Toto African
|
13
|
2
|
6
|
5
|
10
|
15
|
-5
|
12
|
13
|
African Lyon
|
13
|
2
|
3
|
8
|
9
|
20
|
-11
|
9
|
14
|
Polisi Morogoro
|
13
|
0
|
4
|
9
|
4
|
16
|
-12
|
4
|
Kipindi hiki pia kitatoa muda wa mapumziko
kwa wachezaji ambao katika mzunguko mzima wamekuwa wakichua njumu za viatu vyao
kwenye nyasi za viwanja katika juhudi ya kujiweka sawa. Ni katika mapumziko
haya ambapo kutakuwa na mwezi mmoja kuanzia tarehe 15 Novemba 2012 ambao utatoa
nafasi ya Usajili, uhamisho na taratibu zote za mikataba ya wachezaji mpaka
hapo tarehe 15 Desemba 2012.
Wapenzi na wadau wa soka wanasubiri kwa
hamu mwamzo wa mzunguko wa pili wa Ligi kuu itakayoanza tarehe 19 Januari 2012
wakitegemea kuona soka bora zaidi, ushindani na usimamizi bora wa Ligi kuu.
Furaha ya Wapenzi wa soka ni kupata mshindi ambaye atatokana na umahiri na
ueledi wake katika soka. Hivyo mwisho wa ligi hii tarehe 20 Aprili 2012
unategemea kutoa taswira hiyo njema ya soka letu la Tanzania
No comments:
Post a Comment