WEZESHA WANAWAKE

WEZESHA WANAWAKE

Sunday, May 6, 2012

FRANÇOIS HOLLANDE, RAISI MPYA WA UFARANSA!

Raisi Mteule Francois Hollande (57)
Zile mbio za kuwania Kiti cha Uraisi wa Ufaransa zimefikia ukingoni baada ya Nicolas Sarkozy kukubali kushindwa na mpinzani wake bwana Francois Hollande katika Uchaguzi wa kumtafuta Raisi wa Ufaransa katika awamu ya Pili kwa tofauti ya 3.4%. Nicolas Sarkozy ambaye ni Raisi wa 23 wa Ufaransa aliingia madarakani tarehe 16 Mei 2007 na antegemea kuachia madaraka tarehe 17 Mei 2012
Raisi Nicolas Sarkozy (57)
Francois Hollande anatoka katika Mrengo wa kushoto wa siasa za Ufaransa katika chama cha Socialist Party (PS). Alipoanza harakati za kuwania nafasi hii ya juu katika nchi ya Ufaransa kabla ya kashfa ya ngono dhidi Dominique Strauss-Kahn ambaye ndio alionekana kuwa mpinzani makini wa Nicolas Sarkozy, Hollande alionekana kama akipoteza wakati wake.
Raisi Mteule Francois Hollande
Ushindi wa Raisi Mteule Francois Hollande (57) unabadilisha muelekeo wa siasa za Ufaransa kutoka Mrengo wa kulia kwenda kushoto baada ya takribani miaka 20. Ushindi huu unapatikana wakati Ufaransa ikiwa katika jitihada za kupambana na mtikisiko wa Kiuchumi ambao umeiathiri Ufaransa pamoja na nchi nyingine za Ulaya.
Wafuasi wa Raisi Mteule Francois Hollande wakifurahia Ushindi

Kundi la Vijana kutoka katika Chama chaSocialist Party(PS) wakigonganisha Glasi za Mvinyo kufurahia Ushindi 
Raisi anayeondoka madarakani Nicolas Sarkozy, anatoka madarakani baada ya uongozi wa nchi hiyo katika kipindi kimoja na kumfaya kuwa Raisi wa 11 kushindwa katika kinyang’anyiro cha Uraisi katika nchi za Ulaya toka Mtikisiko wa Uchumi ulipoanza mwaka 2008. Pamoja na sababu zingine, wataalamu na wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanaona kuwa Mtikisiko wa kiuchumi umechangia katika kushindwa katika chaguzi mbalimbali kwa Maraisi walioko katika Jumuiya ya Ulaya.
Kwaheri Raisi Nicolas Sarkozy
Baada ya Kukuabli matokeo yaliyompa Ushindi Raisi Mteule Francois Hollande, Raisi Nicolas Sarkozy amewashukuru wafuasi wake na wote waliomsaidia katika kinyang’anyiro cha kuwania Uraisi wa Ufaransa katika awamu ya Pili. Alisema kuwa alijaribu kwa kadri ya uwezo wake kushinda katika kinyang’anyiro hiki lakini ikashindikana. Anajua kuwa wananchi walikuwa na hasira na jinsi ambavyo amekuwa akishughulikia suala la Uchumi wa Ufaransa lakini amekubali kuwajibika kwa matokeo ya Uchaguzi huo.
Aidha Nicolas Sarkozy baada ya kukubali matokeo ya Uchaguzi alimtakia kila la kheri Raisi Mteule Francois Hollande.

Raisi Mteule Francois Hollande aliwashukuru wapigakura wote huku akiahidi kuwa Raisi wa wote, yaani wa waliompigia kura na wale ambao hawakumpigia kura. Alisisitiza kuwa yeye ni mtu wa Kawaida na atafanya kazi kuinua uchumi uliotetereka na kushughulikia ahadi yake ya kusimamia Haki na masuala ya Vijana.Raisi Mteule Francois Sarkozy attanza Kazi rasmi tarehe 17 Mei 2012

Kufuatia Ushindi huo Raisi wa Marekani, Barack Obama, ambaye naye yuko katika harakati za kuwania ofisi hiyo ya Uraisi wa Marekani kwa awamu nyingine, alimpigia simu Raisi mteule Francois Hollande na kumpongeza kwa Ushindi alioupata


No comments:

Post a Comment